Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Sunday, March 22, 2009
HII NDIYO SURA HALISI YA AFRIKA

AFRIKA ni bara linaloongoza kwa kuwa na sura za umaskini hasa ule unaowafanya binadamu kukosa kile alichokiita Abraham Maslow haki za msingi yaani chakula, malazi na mavazi. Nimepita hapa na kukuta taarifa na picha hii ambayo kwangu haijanifurahisha.

Haki chakula ni jambo ambalo nimekuwa nikilizungumza sana na ninatamai siku moja kila mwananchi kwa kuanza na Tanzania apate haki hii ya msingi. Kama tukikubali kurejesha sera za vitendo katika kilimo bila shaka tutamudu kuwezesha watu wetu kupata chakula wakati wote.

tunafahamu kuwa wakishapata chakula kiasi cha kushiba ni jukumu la pili kusisitiza juu ya chakula bora. Wimbo wa chakula bra hauwezi sasa kuimbw ana serikali yetu kwa kuwa hata haki ya chakula tu kwa wananchi bado ni kitendawili. Kuna waziri wa Kilimo nchini anaitwa Wassira, ni maarufu sana kwa maneno matamu lakini utendaji wa wizara hiyo katika kutibu tatizo la upatikanaji wa chakula bado ni ndoto takayohukua siku nyingi kupata jibu. Tunasubiri sijui aje nani ili kuhamaisha kilimo cha chakula katika Afrika? Inakera na kuumiza sana!
 
© boniphace Tarehe 3/22/2009 07:21:00 AM | Permalink |


Comments: 6


   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved