Tarehe 11/22/2006 10:45 PM, Mtoa Maoni: bongozite
Tarehe 11/25/2006 1:56 AM, Mtoa Maoni: Unknown
sielewi vizuri protocol za SADC naona nchi nyingi rais alizoenda kujitambulisha ni SADC na east africa.kitu ambacho kinasikitisha katika safari hizo na za viongozi wetu ni safari za kwenda kuangalia afya zao nje!!!ni nini wanachokifuata kwenye hospitali za nje ambacho wameshindwa kukiweka kwenye hospitali zetu???haya ni madhara ya kutojua tu na pamoja na kasumba,na inakera tena inakera sana.kwa gharama ndogo kuliko za viongozi wote wanaoenda kutibiwa nje kwa mwaka tungeboresha hospitali angaliau moja na ingetibia watanzania wengi zaidi!ee mwenyezi mungu wafungue macho viongozi wetu na wajalie moyo wa huruma.
Tarehe 11/25/2006 9:06 PM, Mtoa Maoni: Rashid Mkwinda
Afanaaleik huyu ndiye Rais tuliyempa kura zetu ameamua kuwa mtalii ilhali wapika kula wake wakiendelea kufa njaa kukosa tiba ya uhakika na baadhi ya akina mama wajawazito wakifa kwa kukosa huduma za uzazi, mie sisemi nikisema nitaambiwa oooh napinga sera za chama twawala za Ari Mpya Nguvu Mpya na Kasi Mpya bila fikra mpya.
Tarehe 11/26/2006 11:07 PM, Mtoa Maoni: mnyalu
Asante sana bwana Makene kwa kuona mbali.
Unajua nimeshaona watz wengi bado hawajajua swala la 'Opportunity cost'. Hivi unawezaje kulipa kipaumbele swala la safari nje ya nje ukiwa rais, kuliko kukaa na viongozi wa ndani na wananchi kutafuta suluhu ya baadhi ya matatizo yanayotatulika. Safari siyo kitu kibaya, lakini kipindi hiki ni kigumu kiuchumi na hata kwa miundo mbinu na nishati katika Tanzania. Nahisi kama rais na baadhi ya wanaozikubali hizo safari, hawaonji shida ya Watanzania iliyopo sasa.
Kibaya zaidi safari anazofanya rais, kama za kutangaza mazingira ya biashara nk, zinaweza kufanywa na waziri Migiro. Au yeye mheshimiwa rais hajajua kuwa yeye ni rais sasa, na si waziri wa mambo ya nje? Shida ya misafara ya rais ni kwamba inagharimu pesa nyingi sana kuliko angemtuma waziri wake. Sababu moja ni msafara wake mkubwa anaofuatana, acha familia yake kama mke na watoto, kuna msululu mkubwa wa wafanya biashara, wanasiasa na viongozi toka ofisi yake.
Nchi kuwa na amazingira mazuri ya uwekezaji hakutangazwi kwa safari tu. Bali ni kuandaa mazingira mazuri. Wenyewe tu wataambizana kuwa Tanzania kunafaa. Kwa taarifa, mataifa ya magharibi na Marekani, yanajua kilichomo ndani ya TZ hata kabla raisa hajasafiri kuwaeleza kuna nini. Wenzetu wanathamini sana habari 'Information is Power' kwao. Hivo wana habari zote za Tanzania, hata kama saa zingine huamua kuzipotosha kwa maslahi yao.
Nadhani rais amekuwa na malengo mengi mno kwa mpigo. Anahisi kila kitu kinaweza kufanyika mara moja namna hiyo. Saa zingine hata nikisikiliza hotuba zake namwona kama shekhe au askofu na waumini wake. Maana anaweza kuongelea tatizo na kuwapa matumaini hata kwa swala ambalo hajui utatuzi wake unawezekana au la.
Sasa rais akiwa mhubiri, raia wanajua kuna kitu hapo? Uzuri alionao ni kwamba anakubalika na watz wengi. Na wengi wao ukiwauliza kwanini wanadhani aanafanya kazi nzuri, hawajui. Ni kama tu kufuata upepo. Kuwa na uchungu na matatizo ya watz peke yake bila kuwa na utatuzi ni kama haisaidii kitu. Namwunga mkono Tegembwage pia, aliyeonya vyombo vya habari kutosifia kazi zinazofanywa na serikali, kwani wanatimiza wajibu wao. Hii inaonesha kuwa tumezoea kuwa na viongozi ,atapeli, kiasi tukipata mtu asiyemwongo, tunajiona tuna bahati, wakati ni haki yetu kuetendewa hayo wanayotenda kama kutimiza ahadi zao.
Naweza kuongea hadi kesho kwani yapo mengi yanayonikera ila sioni kama Tz ni nchi ya kuibadisha siku moja. Ila tunakokwenda hili tabaka litakuja tu kung'olewa. Hata dola imara kama ua Kirumi, Uingereza na zingine, nani alijua kuna siku zitakuja kuwa chini? Ngoja tu muda tutakuja kuona mabadiliko, ni swala tu la muda. Nashukuru wengi sasa wanasoma Tz.
Mwisho, bwana Makene, hizo safari ulizotaja ni badhi tu ya zile alizofanya rais nje ya Tanzania. Mbona sijaona umetaja nchi yoyote ya mashariki ya kati. Nakumbuka alishaenda sehemu kama Uarabuni Saudi na Mwungano wa Falme za Kiarabu (UAE), maeneo ya DUBAI.
ASANTE......KEEP US INFORMED.
Tarehe 11/27/2006 7:55 AM, Mtoa Maoni: Ndesanjo Macha
Tarehe 11/29/2006 8:52 AM, Mtoa Maoni: MICHUZI BLOG
Tarehe 11/30/2006 10:57 PM, Mtoa Maoni: Christian Bwaya
Tarehe 12/03/2006 3:58 AM, Mtoa Maoni: John Mwaipopo
Bonny nimewahi kusoma sehemu fulani kuwa tuziara anatotufanya bwana mkubwa tumeanza kuzaa matunda. sasa sijui ni ileile maneno ya wanamtandao kufagilia na kusifia hata pakiwa pana uwongo. Si unawajua wanamtandao.
Hivi ile enzi ya Nyerere ya kuwatuma mawaziri kwenda nje kwa shughuli hizi hizi haitarejeaga tena eti.
Tarehe 12/11/2006 1:51 PM, Mtoa Maoni: MICHUZI BLOG
Tarehe 12/16/2006 5:14 AM, Mtoa Maoni: Sultan Tamba
Kutembea tembea ndiyo staili aliyoingia nayo Mkuu wetu wa awamu ya nne. Au Mmesahau Mzee Mkapa alivyoingia alikuja na staili gani? Ntawakumbuka; yeye aliingia na mkwala wa kutoa hotuba bila kusoma kwenye makaratasi! Popote pale anabonga tu! Kama Nyerere! Matokeo yake akajikuta anakanusha maneno yake mwenyewe kwenye vyombo vya habari mara tano mfululizo! Magazeti yakamchora katuni, yakasema sasa rais wetu anakaribia kuingia kwenye kitabu cha Guinness kwa tabia yake ya kukanusha kanusha maneno yake! Kuanzia hapo akaacha! Kila hotuba, anasoma katika karatasi! Nna wasiwasi hata alipokuwa akialikwa kwenye bethdei akiambiwa atoe mawili matatu! Anafungua karatasi, anasoma!
Na Kikwete ataacha tu! Msiwe na wasiwasi!!
Tarehe 6/13/2015 1:23 PM, Mtoa Maoni: imanauliya
Nice blog and article, thanks for sharing. However want to statement on few common issues, The website taste is great, the articles is in point of fact excellent
Pembuatan Vimax
Penambah Gairah Sex
Mengatasi Masalah Seksual Pria
Cara Memperbesar Alat Vital Pria
Pembesar Alat Vital Pria
Penemuan Vimax Canada
Komposisi Bahan Vimax
Vimax Pills
Obat Atasi ejakulasi dini
Obat memperbesar Alat Vital
Vimax memperbesar Penis Alami
Jual Vimax
Cara memuaskan istri di ranjang
Obat Memperbesar Penis Alami
Penyebab disfungsi ereksi
Cara memperbesar Penis
Jual Vimax Asli
Manfaat Hubungan Seks
Tentang Vimax kapsul
Obat Pembesar Penis
Hizi ziara zote pia zinasaidia sana kupromote Tanzania. Magazeti ya nje yataandika kuhusu Tanzania na ziara ya raisi. Wafanya biashara ambao wanaweza kuekeza na kuona opportunities watakimbilia Tanzania. Touarism inapata promotion moja kubwa sana. Tanzania inajulikana kwa umasikini sasa ziara za raisi zianondoa hiyo na kuionyesha tanzania kama ni nchi ya uwezekano, maendeleo na nchi nzuri ya mapumziko.