Saturday, October 14, 2006
NAMKE NDIPO NISEME?
NAMKE ndipo niseme
Nishike jembe nilime
Mdomo nisiachame
Na macho yasitazame?
Nilie nikichekea
Watu wasijejulia
Nicheke nikililia
Umati furahishia?
Nandike bila somea
Nikopi walosemea
Nisome walofutia
Ukweli taupatia?
Nikue bila julia
Nilale bila otea
Nisene bila wazia
Hayawani niitiya?
Utoto lini achia
Ukubwa lini fikia
Kumbukumbu kujulia
Muhimu kwa walofia?
Ni mwaka naukatia
Langu tando fungulia
Mwadhani litadumia
Mawimbi kuyashindia?
Sitaki kujisifia
Mtoto sijatembea
Ni lini nitasemea
Siku nitapofilia?
Nyamongo kalizaliwa
Mwisenge akapitia
Mabui akaishia
Na Nyasho kitembeleya!
Kienda Ihungo Piya
Matoke kutafuniya
Nadanda akatimkiya
Mkwawa akihamiya.
Kikafika Dasalama
Tiesijii someya
Kalamu kikashikiya
Mlimani kupandiya!
Kisha hitimu ilimu
Na kupata unajimu
Amerikani jihimu
Mataifa jifyunziya!
Huko kikaanzishiya
Gazeti Tando la umma
Kasri kaliitiya
Mwaka moja wapitiya!
Nini anachotakiya
Kama si kulaliya
Siku ajapo filiya
Mwili tu poteleya!
© boniphace Tarehe 10/14/2006 02:32:00 AM
|
Permalink |
-
Makene,
Nimekubali.Ushairi mzuri sana huu,maneno haya wanayasikia?
-
Hongera mshairi! Ujumbe una njia nyingi za kuufikisha. Hata hivyo watu wako masikio wazi na macho mita mia moja kuangalia! Usishangae kesho ukasikia shairi lako watu wanaliimbia taarabu!!! Hongera! Nimelipenda na ujumbe wake.
-
KAKA HII BETI YA USHAIRI INANIKUMBUSHA SANA HAYATI PEPE KALE ALIVYOJIIMBIA MWIMBO WA KUJIAGA: Nini anachotakiya
Kama si kulaliya
Siku ajapo filiya
Mwili tu poteleya!
-
Sema ulojifunzia, kwa kalamu kushikia,wafunze wenzio pia,ukumbukwe kijifia, hazina uloachia, vilembwe kunakiria, kazizo nafurahia, zaduru bara baharia.
-
Nini kuimbia taarabu amenikumbusha Bw.Tamba hawa vijana wa kizazi kipya ndio haswa watakuwa wa kwanza kunakiri kikubwa ni kwamba hawataki kuketi chini kujifunza ngano hizi kwa malenga walobobea watu wa aina hii wakijififia na hazina itapotea kama walivyojifia akina Shaaban Robert na hazina zao kuhondhiwa sidhani kama familia inanufaika? labda tumuulize Ikbal Shaaban Robert mwana wa mwisho wa mzee Shaaban ambaye nilikuwa namuona akiibuka na baadhi ya mashairi ya babaye magazetini zijui ndio urithi aliopewa wa kunakiri kazi za babaye bila kunoa ubongo wake hilo mie sijui msije kunisuta.
Kazi nzuri sana hii imetulia muala wake vina na mizani vimejipanga vyema huku ujumbe ukisawiri mandhari ya shairi lako.
Marhabaa ndugu yangu kaza msuli safari ni ndefu kuelekea kujikomboa katika fani ya fasihi simulizi na andishi
Wakatabahu
Makene,
Nimekubali.Ushairi mzuri sana huu,maneno haya wanayasikia?