Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Monday, July 10, 2006
MWANAZUO SETH CHACHAGE AMETUTOKA

KASRI LA MWANAZUO limepokea taarifa za kuondoka kwa mmoja wa wanajamii wa Wanazuo wa Tanzania kwa masikitiko. Kama umewahi kusoma "Makuwadi wa Soko Huria" riwaya mpya kabisa inayojadili ubinafsishaji basi utamfahamu Profesa Seth Chachage ambaye kwa taarifa nilizozipata tangu jana amefariki dunia.

Mara ya mwisho KASRI lilipata fursa ya kufanya mahojiano na Profesa huyo na kwa heshima yake mahojiano haya yataandikwa katika safu ya Gazeti la Mwananchi na kisha kuwekwa hapa baadaye wiki ijayo. Nina mengi ya kuandika kuhusu gwiji huyu lakini niishie hapa kuwapa taarifa wanajumuiya ya wamiliki wa Magazeti Tando maana Chachage katika siku za uhai wake amechangia sana kuikuza jamii yetu kwa kuhamasisha msingi wa kumdharau mnyonyaji na kuongeza ujasiri kwa wanaonyanyaswa! Kama unakumbuka sana hili ndilo lengo kuu na msingi wa jumuiya yetu.

Poleni wanazuo wote na nitumie fursa hii pia kutoa pole kwa familia ya Marehemu na jumuiya ya Chuo Kikuu Dar es Salaam. Ni ukweli ulio wazi kuwa Chachge amevipiga vita vilivyo vikali na kwa kiwango kikubwa amevishinda na anapumzika kwa heshima!

Bwana ametwaa na siku zote hakuna anayeweza kuhoji uhalali wa hulka yake njema!

Pichani anaonekana Chachage akiwa katikati katika moja ya makongamano mbalimbali aliyofanya wakati wa uhai wake.
 
© boniphace Tarehe 7/10/2006 10:04:00 AM | Permalink |


Comments: 7


  • Tarehe 7/11/2006 6:14 AM, Mtoa Maoni: Blogger John Mwaipopo

    Kweli yametimia.

    Niliwahi kukorofishana naye wakati nikiwa rais wa kitivo cha fani na sayansi za jamii na yeye akiwa dean msaidizi wa kitivo hicho.

     
  • Tarehe 7/11/2006 7:36 AM, Mtoa Maoni: Blogger Egidio Ndabagoye

    Mungu amlaze mahali pema peponi amina.

     
  • Tarehe 7/12/2006 7:22 PM, Mtoa Maoni: Blogger Jeff Msangi

    Hili ni pigo la taifa.Kwa bahati mbaya nchi zetu huwa hazina utaratibu mzuri wa kuenzi watu kama hawa na haswa kazi zao za kitaaluma.Badala yake wanasiasa ndio huonekana watu kuliko magwiji kama marehemu Chachage.Kimsingi taifa na nyanja nzima ya elimu Tanzania imepoteza mtu wa maana sana.Mungu ailaze mahali pema peponi roho yake.

     
  • Tarehe 7/13/2006 4:51 AM, Mtoa Maoni: Blogger Christian Bwaya

    Nina riwaya yake ya Sudi ya Yohana kama kumbukumbu yake.

    Habari hizi ni za kusikitisha. Tanzania imemkosa mwanaharakati muhimu sana.

     
  • Tarehe 7/13/2006 6:01 AM, Mtoa Maoni: Blogger mloyi

    Ametutoka, ingawa wengi huku uswahilini walidhani yeye ni msema ovyo lakini alisaidia sana watanzania kujua makosa yanayofanywa na serikali.
    Hakupewa nafasi ya kufuatiliwa mawazo yake hivyo hatuwezi kumkosoa sana.
    Harakati amesema hatuna utaratibu wa kuenzi watu kama yeye, sijui sisi tutauenzi vipi mchango wake? na sio kuuenzi kama njia ya kuchangishia watu pesa bali kuwasaidia kuboresha maisha yao.
    Tunaomba waliomtangulia wamkaribishe kwenye makazi ya milele kwa amani.

     
  • Tarehe 7/18/2006 5:53 AM, Mtoa Maoni: Blogger mzee wa mshitu

    He Makene tumepoteza sana

    Kwa kweli hili ni pigo kubwa sana sijui nisemeje lakini tumeumia kukosa mtu mwenye mtizamo mpana sana katika masuala ya jamii ambaye hakutaka kupindishwa na modernization. Hakupenda utandawizi. alichukia sana Nothing is Going On (NGO) alifanya mengi kutetea walalahoi ingawa alikuwa na uwezo wa yeye kujigeuza 'mungu mtu'

     
  • Tarehe 7/19/2006 5:01 PM, Mtoa Maoni: Blogger Ndesanjo Macha

    Unajua ni cheche za watu kama Chachage ambazo zimetufanya wengine kuwa na fikra kama tulizonazo. NI huzuni kuwa ametutoka ila ni huzuni pia kwakuwa sidhani kama taifa lilimwonyesha waziwazi jinsi gani amekuwa na mchango mkubwa nchini katika nyanja za taaluma, fasihi, na maendeleo. Makene, umetuwakilisha wanablogu kwa makala mfululizo kuhusu mwanataaluma huyu.

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved