Tarehe 7/11/2006 6:14 AM, Mtoa Maoni: John Mwaipopo
Tarehe 7/11/2006 7:36 AM, Mtoa Maoni: Egidio Ndabagoye
Tarehe 7/12/2006 7:22 PM, Mtoa Maoni: Jeff Msangi
Hili ni pigo la taifa.Kwa bahati mbaya nchi zetu huwa hazina utaratibu mzuri wa kuenzi watu kama hawa na haswa kazi zao za kitaaluma.Badala yake wanasiasa ndio huonekana watu kuliko magwiji kama marehemu Chachage.Kimsingi taifa na nyanja nzima ya elimu Tanzania imepoteza mtu wa maana sana.Mungu ailaze mahali pema peponi roho yake.
Tarehe 7/13/2006 4:51 AM, Mtoa Maoni: Christian Bwaya
Tarehe 7/13/2006 6:01 AM, Mtoa Maoni: mloyi
Ametutoka, ingawa wengi huku uswahilini walidhani yeye ni msema ovyo lakini alisaidia sana watanzania kujua makosa yanayofanywa na serikali.
Hakupewa nafasi ya kufuatiliwa mawazo yake hivyo hatuwezi kumkosoa sana.
Harakati amesema hatuna utaratibu wa kuenzi watu kama yeye, sijui sisi tutauenzi vipi mchango wake? na sio kuuenzi kama njia ya kuchangishia watu pesa bali kuwasaidia kuboresha maisha yao.
Tunaomba waliomtangulia wamkaribishe kwenye makazi ya milele kwa amani.
Tarehe 7/18/2006 5:53 AM, Mtoa Maoni: mzee wa mshitu
He Makene tumepoteza sana
Kwa kweli hili ni pigo kubwa sana sijui nisemeje lakini tumeumia kukosa mtu mwenye mtizamo mpana sana katika masuala ya jamii ambaye hakutaka kupindishwa na modernization. Hakupenda utandawizi. alichukia sana Nothing is Going On (NGO) alifanya mengi kutetea walalahoi ingawa alikuwa na uwezo wa yeye kujigeuza 'mungu mtu'
Tarehe 7/19/2006 5:01 PM, Mtoa Maoni: Ndesanjo Macha
Unajua ni cheche za watu kama Chachage ambazo zimetufanya wengine kuwa na fikra kama tulizonazo. NI huzuni kuwa ametutoka ila ni huzuni pia kwakuwa sidhani kama taifa lilimwonyesha waziwazi jinsi gani amekuwa na mchango mkubwa nchini katika nyanja za taaluma, fasihi, na maendeleo. Makene, umetuwakilisha wanablogu kwa makala mfululizo kuhusu mwanataaluma huyu.
Kweli yametimia.
Niliwahi kukorofishana naye wakati nikiwa rais wa kitivo cha fani na sayansi za jamii na yeye akiwa dean msaidizi wa kitivo hicho.