Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Friday, April 07, 2006
SASA NI KIBANDA ANAYEINGIA
MWANANCHI kumewaka moto, kila mwandishi anatakiwa kumiliki Gazeti Tando kabla mtandao wa Magazeti yanayochapishwa na kampuni hiyo haujakamilika na kuwekwa katika intenet. Absalom Kibanda mmoja wa wachambuzi wa juu kabisa wa masuala ya kisiasa katika Tanzania, mwenye uzoefu wa fani ya uandishi kwa miaka mingi naye ameitikia wito wa kufungua gazeti tando lake lisome hapa.

Halafu kama umempitia Msangi Mdogo utakuta kuna mapinduzi haya ambayo ameyaleta MK wa vijimambo. Wakati huo huo nashawishika kuamini kuwa anayetengeza mitandao ya blog za Tanzania anazidiwa kete kwa kuwa kama unatazama Athuman kapotea mtandaoni bila taarifa za kiufundi kutolewa.

Lakini haijatosha kuna mtanzania halisia ameingia pia mtembelee hapa. Huyu na mwingine sijui nani! Hapana nataka kumsalimu Mark Msaki na ndugu yangu Miruko kwa kubadili nyumba yake. Mapinduzi haya yananipa swali la kuhoji ni wapi mnapata mali hizi nyingi za kujenga mahekalu mtandaoni huku mimi ka kasri kangu kakibaki vile vile. Tunahitaji kuchunguza jitihada hizi za MK na kumpongeza maana sasa Magazeti Tando yetu yanapokelewa na kutanuka kwa kasi ajabu. Hureeeee asiye na mwana alale sisi Mwananchi tunazidi kupumua tuu. Wenye wivu ajinyonge! Charahani tunashukuru sana jitihada zako.
 
© boniphace Tarehe 4/07/2006 09:06:00 AM | Permalink |


Comments: 3


  • Tarehe 4/07/2006 9:36 AM, Mtoa Maoni: Blogger MICHUZI BLOG

    gazeti tando ndo nini vile?

     
  • Tarehe 4/08/2006 2:32 AM, Mtoa Maoni: Anonymous Anonymous

    Asante kwa kutaarifu habari njema hizi.

     
  • Tarehe 4/08/2006 8:52 AM, Mtoa Maoni: Blogger ARUPA

    Ili ujenge hekalu kubwa na zuri tafuta matofari ya kuchoma yanauzwa kwa wingi na msangi mdogo, ili ujenge hekalu zuri uachane na ka kasri kako kadogo kama kibanda

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved