Tarehe 4/11/2006 5:38 AM, Mtoa Maoni: mwandani
Tarehe 4/11/2006 7:18 AM, Mtoa Maoni: Christian Bwaya
Makene,
Nashukuru sana kwamba teknolojia hii inaweza kutupatia mambo makubwa namna hii. Nimekuwa nikiifuatilia tangu ilipoanza ingawa sikuacha maoni. Kimsingi nina mengi sana ya kusema kuhusu Barua hii nzito ambayo imeibua mijadala isiyorasmi miongoni mwa vijana wenzangu.
Naomba kujua iwapo naweza kuichapa na kuifikisha kwa watanzania wenzako hapa nyumbani ili mjadala uwe mzuri zaidi. Suala la haki miliki katika mtandao sina ujuzi nalo.
Tarehe 4/11/2006 9:16 AM, Mtoa Maoni: boniphace
Mwandani shukrani, bora kunywea kikombe changu kuliko kukimbia mvinyo huu. Kikombe hiki nakishika lakini kigumu naona umeona hata wewe ila mapenzi ya baba aliyenituma yatime.
Bwaya malengo ya Mgazeti Tando ni kufikishia taarifa umma mkubwa bila vizingiti. Ruksa wachapie na kuwafikishia maana imani yangu kuwa hakuna mtunzi atakayeweza kutunga haya maisha yangu. Ni mimi tu, maana asilimia kubwa ya barua hii ni ukweli na subiri mengi yanakuja.
Makene
Tarehe 4/12/2006 4:53 AM, Mtoa Maoni: mzee wa mshitu
Makene
Uchungu huu unaweza ukatufanya vijana tukashika mapanga na mashoka twende tukawakomboe mama na baba zetu waliopo kule Namagondo na kwingineko inatia uchungu inasikitisha. Tuhabarishe!
Inawezekana miongoni mwetu tunaona ona tu halafu tunasahau, hatutilii maanani huenda mambo kama haya yakainua ari na nguvu mpya.
Makene naona una machungu, akisha yasoma yote haya, mama ataweza kustahimili ukweli huu?
Na kama tutamtaka huyo mama awe na heri na maisha marefu si itakubidi ufiche ukweli huu?
Lipi rahisi?
Kazi safi, tena inaamsha hisia.