BARUA imefika sehemu ya nane inayojadili maisha ya vyuo vikuu vya Tanzania na mfano chuo Kikuu Dar es Salaam. Nafasi ya serikali za wanafunzi namasaibu yake. Endelea kusoma sasa hapa sehemu hii ya nane.
Makene, Ijumaa kuu imenipa fursa ya kusoma nyaraka zako kwa kina. Sijasoma hii sehemu ya nane, nimeanza kusoma tangu sehemu ya kwanza kwa mara nyingine tena na ndio kwanza nimalize sehemu ya pili ya barua hii.
Barua hii imenigusa, haswa sehemu ya pili unapomzungumzia mama kama mwalimu. na miye mama yangu alikuwa ni mwalimu, tena katika shule niliyosoma kama wewe, na mimi mama yangu alinichapa ili kuonyesha mfano kuwa hana upendeleo.
Barua yako inanigusa roho kwa sababu nadhani japo ni ya kubuni ina ukweli mwingi sana ndani yake.
Inanikumbusha kitabu cha mwanaharakati wa haki za watu weusi huko Marekani, George Jackson: The Soledad Brother.
Kitabu hicho kilikuwa ni mkusanyo wa barua alizoziandika kwa familia yake na marafiki akiwa gerezani San Quentin. Kana kwamba ni za kubuni, barua hizo zilikuwa ni barua zenye mchomo mkali sana, Nakushauri ukisome kitabu hicho kama bado hujakisoma.
Nakupa heko na hamasa: ENDELEA KUANDIKA. Kwani unawakilisha mawazo ya "Post indepenndence, post one party state Africa" Kama Ngugi alivyosema kwenye kitabu chake cha insha za: HOMECOMING
"A writer responds, with his total personality, to a social environment which changes all the time. Being a kind of sensitive needle, he registers, with varying degrees of accuracy and success, the conflicts and tensions in his changing society. Thus the same writer will produce different types of work, sometimes contradictory in mood, sentiment, degree of optimism and even world view. For the writer himself lives in, and is shaped by, history."
Naam, nimezisoma habari za kukanywa na mama yako - mama yangu pia bila ya shaka - Nimezisoma dhiki zilizowakabili waalimu wa wakati wa mama yako - mama yangu pia. Nimezisoma habari za TAMWA - African feminism. Nasema tena ENDELEA> Wakilisha kizazi chetu.
bonny, unaweza kuwa shakespear wetu kiutani utani tu. unajua hivi sasa hatuna tena kina kezilahabi, na hawa kina senkoro waliopo hawatoshi na wahitahika wengine wengi wapya? kaza buti kaka, fanya kweli... na hongera kwa kipaji cha kutisha
Makene, Ijumaa kuu imenipa fursa ya kusoma nyaraka zako kwa kina. Sijasoma hii sehemu ya nane, nimeanza kusoma tangu sehemu ya kwanza kwa mara nyingine tena na ndio kwanza nimalize sehemu ya pili ya barua hii.
Barua hii imenigusa, haswa sehemu ya pili unapomzungumzia mama kama mwalimu. na miye mama yangu alikuwa ni mwalimu, tena katika shule niliyosoma kama wewe, na mimi mama yangu alinichapa ili kuonyesha mfano kuwa hana upendeleo.
Barua yako inanigusa roho kwa sababu nadhani japo ni ya kubuni ina ukweli mwingi sana ndani yake.
Inanikumbusha kitabu cha mwanaharakati wa haki za watu weusi huko Marekani, George Jackson: The Soledad Brother.
Kitabu hicho kilikuwa ni mkusanyo wa barua alizoziandika kwa familia yake na marafiki akiwa gerezani San Quentin. Kana kwamba ni za kubuni, barua hizo zilikuwa ni barua zenye mchomo mkali sana,
Nakushauri ukisome kitabu hicho kama bado hujakisoma.
Nakupa heko na hamasa: ENDELEA KUANDIKA. Kwani unawakilisha mawazo ya "Post indepenndence, post one party state Africa"
Kama Ngugi alivyosema kwenye kitabu chake cha insha za: HOMECOMING
"A writer responds, with his total personality, to a social environment which changes all the time. Being a kind of sensitive needle, he registers, with varying degrees of accuracy and success, the conflicts and tensions in his changing society. Thus the same writer will produce different types of work, sometimes contradictory in mood, sentiment, degree of optimism and even world view. For the writer himself lives in, and is shaped by, history."
Naam, nimezisoma habari za kukanywa na mama yako - mama yangu pia bila ya shaka - Nimezisoma dhiki zilizowakabili waalimu wa wakati wa mama yako - mama yangu pia. Nimezisoma habari za TAMWA - African feminism. Nasema tena ENDELEA> Wakilisha kizazi chetu.