Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Saturday, April 08, 2006
AZIMIO LA DODOMA NA MUELEKEO WA MAGAZETI TANDO YA KISWAHILI
MARK Msaki ametoka Afrika Kusini na kufika Dodoma kutekeleza jukumu la kupitisha Azimio la kutathimini taswira ya wamiliki na waandishi wa Magazeti Tando ya Kiswahili (Blogu). Safari hii ni ya pili kupata kuandikwa, ya kwanza ni ile Kasri alipoweza kukutana na HARAKATI pale jijini Toronto. Kumekuwa sasa na mazungumzo ya wana magazeti Tando kila pande ya dunia. Jumuiya hii sasa inakuwa kwa kasi sana na hatukutarajia iwe hivi mapema. Kama mzazi unapoongeza mtoto ni jukumu lako kutafuta kitanda kipya. Kutokana na ukweli huu nasi tuna jukumu la kutafuta maadili yetu na tayari AZIMIO LA DODOMA limepitishwa na hili chini ya Mwenyekiti KURUNZI na katibu wake MIRUKO na mjumbe mwenye heshima iliyotukuka MARTHA na komredi HUDSON KAZONTA. Kasri anapongeza na kulikubali Azimio hili. Jitihada hii sasa inatupa picha kuwa baada ya siku si nyingi Magazeti Tando yatakuwa yakisomwa katika redio asubuhi na pia jumuiya yetu inaelekea kuzuri ambapo hata tuzo za mwaka zitafuatia hivi karibuni. Yote haya ili yafanikiwe yanahitaji wafanikishaji. Lazima kuwe na uongozi wetu wa kutuunganisha. Kamati ya Muda imepatikana na sioni sababu ya kuivua madaraka sasa hadi tutakapoamua vingine. Nikupongezeni na kukuombeeni pumzi ya mola muweze kutufikisha safari ya matarajio yetu. Asanteni, naomba kuwasilisha.
 
© boniphace Tarehe 4/08/2006 09:11:00 AM | Permalink |


Comments: 2


  • Tarehe 4/09/2006 5:47 AM, Mtoa Maoni: Blogger Reggy's

    Asante sana kwa heshima uliyotupatia. wakati tunajadili na kutoa azimio la Dodoma, hakuna kati yetu aliyedhani tunafanya jambo kubwa namna hii. Nawashukuru kwa kulipokea na kulichapisha.

     
  • Tarehe 4/09/2006 12:37 PM, Mtoa Maoni: Anonymous Anonymous

    Sio siri Makene azimio hili linaonyesha jambo muhimu mno: linaonyesha jumuiya hii, ingawa inaweza kuingiliwa na akina "anonimasi," ina watu ambao wanaichukulia kwa umakini wa kila namna na wako tayari kuhakikisha kuwa inasimama na kuwa na maadili yake na mwelekeo wa maana. Tuwashukuru sana ndugu zetu hawa. Na pia wengine, kama ulivyofanya Makene, waliweke kwenye blogu zao na pia kwenye sehemu ya viungo.

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved