Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Thursday, March 16, 2006
SIJUI MTORI AU VIPI, NA MIMI NATAKA!
Ee bwana hii supu ilipikwa kwa saa nyingi kidogo kisha ikawa tamu sana. Lakini kapilipili kalikuwa kakali maana kalinitesa sana kuibugia. Enewei hii sijui niifananishe na supu ya wapi maana mimi Bongo si mtaalamu wa supu kama Fikra Thabiti ambaye alikuwa anatoroka shule kwenda kusaka thupu Kibororoni.

undefined
 
© boniphace Tarehe 3/16/2006 04:34:00 PM | Permalink |


Comments: 4


  • Tarehe 3/18/2006 6:00 PM, Mtoa Maoni: Blogger John Mwaipopo

    Hii maneno ya 'mtori' unafaa uwa-ge makini kuiandika hovyo maana watukumbusha mbali. Kiasili mie sio mla mtori. Nilipokuwa nauona ukitengnezwa na wenye asili nao kule Mbeya nikawa naunyanyapaa lakini siku nilipouonja mara ya kwanza pale Mlimani ndio nilipotambua kuwa ukitaka raha ya ngoma uingie na ucheze. Kunako mtori hunitoi hasa ile asubuhi ambayo jana yake 'ulizikamata' sawasawa (you know what I am saying, I bet so). Nafikiri Ndesanjo na Msaki wameshasahau hata unatengenezwaje.

     
  • Tarehe 3/19/2006 1:59 PM, Mtoa Maoni: Blogger Mija Shija Sayi

    Mzee Makene naona hadi kiti kilikuwa hakikaliki...

     
  • Tarehe 3/22/2006 4:58 AM, Mtoa Maoni: Blogger Fikrathabiti

    Makene hiyo ni supu ya UTUMBO kama ile uliyokua umeizoea sheratoni ya UDSM au????

     
  • Tarehe 3/23/2006 7:04 AM, Mtoa Maoni: Blogger Rashid Mkwinda

    E bwanae mie hapa mate yananidondoka tu ukichulia sikupata staftahi, na mchana umepita bila kutia kitu kinywani, naona kama nikunyang'anye vile hilo bakuli du unafaidi au ni supu ya kitimoto nini mbona naona kama ni nyeupe hivi? astaghfirullah!!!!

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved