
NIMEKUTANA na habari kadhaa baada ya kupitia tovuti za vyama vya siasa. Nitaandika makala haya baadaye. Leo kubwa ni hili na kipicha hiki kinachoelekeza wanaotaka kuwania ubunge na udiwani kupitia chadema, kuwa na kipicha hiki chenye mikuki miwili. Huko juu kuna habari kuwa hakuna kulala hadi kieleweke! Haya maneno si yangu waweza soma zaidi katika tovuti ya CHADEMA hapa na kisha kujibainishia ukweli mwenyewe.
Ni muhimu kukumbuka kuwa CHADEMA kimekuwa kikitumia alama za kitaifa zinazotumika kuonyesha utaifa. Mfano nyuma ya picha ya aliyekuwa mgombea wa chama hicho, kulikuwa na bendera ya taifa. Helkopta iliyokuwa inatumika, ilipakwa rangi za bendera ya Taifa.
Nadhani ndio maana wametumia alama hiyo unayoisema Bwana Kasri. Utakumbukuka katika nembo ya Taifa, kuna mkuki. Sikumbuki alama hiyo katika nembo ya Taifa ina maana gani. Ningejua basi ningefahamu kwa nini CHADEMA, chama cha siasa katiak Tanzania, kimetumia alama hiyo.