Tarehe 3/19/2006 6:46 PM, Mtoa Maoni: John Mwaipopo
Tarehe 3/20/2006 9:16 AM, Mtoa Maoni: FOSEWERD Initiatives
nisiliache hili lipite hivi hivi. ninausifu mtiririko wa hiki kisa...kuanzia na kule kwenye suala la anonimasi kushindwa kuchuja mawazo yao kabla ya kusema...kila mtu huwaza vitu, huanza na kufikiri na mwisho kutoa vitu hadharani, vitu ambavyo vitamsema yeye ni nani...na anataka nini (kama ulivyoainisha baadaye)...hivyo ndivyo baada ya muda vitawafanya wanadamu wengine kupata mahali pa kujenga uwezo, kutetea, kutetewa n.k. mawazo na uwezo wa kufikiri ni hazina, uwezo hujengwa, mara nyengine kupitia shule, au matukio(kula chumvi), au wa kuzaliwa..hatima yake tunautumia uwezo huo kujiendelea sisi kama jamii ya wanadamu...je Einstein aliyegundua matumizi ya Nuclear angeyaficha kapuni, leo hii tungeona mapinduzi yaliyopo katika nyanja za nishati? je aliyegundua injini na mungine akatumia kanuni hizo hizo kuendeleza hadi likatokea gari, mashine ya kusaga, meli na hata baadaye ndege ..... wangekuwa wamejengwa kwenye concepts za uchoyo, tungeweza kuwepo hapa tulipo kama wanadamu???
mapambano ya kifikra ni kitu cha muhimu sana, na lazima kiheshimiwe, kwa mfano ni nani huathiri system? je mwanzo wa kila kitu huwa ni mkubwa? (umeishasema teyari kuwa hata mtoto ataanzia alipoachia baba)....kitu ninachokiona hasa kwa wananchi na wanablogu, ni kuwa je kwa sababu sisi tuliteseka bila sababu ya msingi na watoto wetu wateseke hivyo hivyo? je tuache mambo yaendelee kuharibika na sie tupige makofi? je tunawezaje kumuepusha binadamu na machungu? hasa zaidi wale waliokwenda ughaibuni wanafikiria je, ni laana gani tumepigwa kule nyumbani? hii huuma zaidi baada ya kujifunza kuwa uharibifu unaotokea huko nyumbaniu unatengenezwa na sisi wenyewe!!!!
tofauti na kizazi kilichopita ambacho kinaangalia kupona wao tu, fullstop, kizazi cha sasa huwezi kidanganya kirahisi, kizazi hiki kinaelewa kuwa hata kama unatembelea "Prado" na homu kwako ni raha masaa 24, bado kuna mjomba, shangazi, jirani ambao wanateswa bila sababu za msingi, kwa sababu tu fulani ndiye ameamua iwe hivyo, kizazi hiki kinapiga picha kule kilipotoka na kinapokwenda... kina uzoefu ... kwa ujumla hakitaki makosa yarudiwe....kizazi hiki kimeona wengine wanavyoishi kwenye nchi zao, kimeona uzalendo wao, je nyumbani kunani???
lakini basi kama ilivyosemwa ni kwamba kuna haja ya kuongeza kasi ya kuelimisha raia ili basi wawe wanatumia fursa chache zilizopo kujenga na si kubomoa. uhuru wa kusema kutoa maoni au kuamua unapotumika vibaya ndio chanzo cha kufikiri kuwa kuna umuhimu wa kunyamazisha kundi fulani ikibidi kutumia nguvu ili mambo yaende sawa....umeishasema mfano kundi la wanamtandao wakakamata madaraka, ili kurekebisha mambo (tuombe ibakie kuwa hivyo)....
ukweli lakini unabakia. ni lini Watanzania tutapenda kuwa serious na matatizo yanayotukabili? mbona tukiwa bado wakubwa michezo ya chekechea tunaipenda? je tunamtambua adui wetu kweli? ninahisi na ninateseka sana kama sio kuona tabu, nikifikiria siku utandawazi utapopanda chati bongo!! watu hawataki wala kujiandaa kwa hilo!! hadi leo wanagombana kule mbagala eti "Yesu na mohhamad SAW nani zaidi"!..ninadhani hawa wanaotukana basi tuwaonee huruma na tusijibishane nao...watakuja kugundua kuwa wanachofanya si sahihi... na watajifunza kuargue, pia jinsi ya kutumia fursa chache kwa umakini kutoka kwa wengine
Tarehe 3/21/2006 4:18 AM, Mtoa Maoni: nyembo
Tarehe 3/21/2006 11:59 PM, Mtoa Maoni: Fikrathabiti
Ndugu wanablog wenzangu wenye majina na hekima katika kuchanganua hoja na kutoa mchango mahsusi katika makala za watu, hili wimbi la kuongezeka mijadala ya kashfa katika makala inayofanywa na watu wasio na majina inanitia wasiwasi.
Inakua vigumu kuamini mtu mwenye akili timamu anaweza kukaa na kutumia mda wake kuandika mambo yasiyo na msingi wowote katika jamii.Nikiwa naamini kua wenye busara bado mnatafakari hatua za kuchukua dhidi yao ili kulirudishia heshima gazeti hili tando tarajiwa inabidi tuendelee kua wavumilivu ili kuepusha majibizano na hao wendawazimu yasiyo na mantiki yoyote.
Tarehe 3/22/2006 11:46 AM, Mtoa Maoni: Jeff Msangi
Makene,
Ulichokiandika hapa ni kitu muhimu sana.Nikisema nakupa hongera itakuwa kama huko nyuma ulikuwa huandiki kama hivi.Kuchelea fikra hizo mimi nitakuambia mwendo ni ule ule ingawa kuongeza spidi sio vibaya.
Nimefuatilia kwa kiasi hoja zinazotolewa na hao kina anyonimous.Zingine kwa kweli zinakera kwa sababu sio tu hazitusogezi hata hatua moja mbele bali zinakatisha tamaa vichwa vyenye dhamira njema.Lakini kwa bahati mbaya kabisa dunia si dunia bila mchanganyiko huu.Na siku hizi dhana ya uhuru wa habari ndio changamoto yetu mpya..yaani habari na maoni bila mipaka.Cha muhimu sana ni mimi na wewe kutambua wajibu na nafasi yetu katika jamii.Hapo ndipo panapokuwa na maji kujitenga na mafuta.Uhuru wa habari na mawasiliano usikukere hata kidogo.Kama unavyosema,cheza karata yako.Haya mengine ni pumba katika mchele!
Umeongea mengi mema kama kawaida yako Bonny lakini la msigi ni hili la hawa Anonimasi. Hakika wamenipa changamoto sana juu ya sura yangu na maoni yangu kule kwenye kibaraza cha michuzi. Hivi sasa nimeshapata dawa -cream- ya kujipaka na kujichubua huenda nikawa mzuri kama watakavyo wao na sio yeye aliyeniumba. Sikujua kuwa vibaraza hivi ni vya kuchangia hoja na masuala jadidi. Kumbe ni mashindano ya ama urembo ama kujificha mithili ya askari wa mwituni.
Lililonikera sana ni kuingilia mawazo ya mtu mwingine ambayo hata hayadhihaki mtu. Mathalani lugha na nakshi ambazo ndani yake hayana ukakasi bali sanaa na weledi wa namna fulani. Mwenye blogu mwenyewe ndiye alihamasika kunisabahi kwa kiluga changu (bahati njema anazungumza lugha karibu 10 hivi- hili aliniandikia mwenyewe). Akiandika yeye vema nikimjibu nongwa.
Kazi ipo na inahitaji busara na uvumilivu kama Mark Msaki na Ndesanjo walivyonena kule kwa bwana Muhidin.