Tarehe 3/27/2006 1:20 PM, Mtoa Maoni:
Tarehe 3/30/2006 9:44 PM, Mtoa Maoni: mzee wa mshitu
Makene huyu mamake Kasri ni amenikumbusha mbali sana sawa na mamake Mzee wa Mshitu akiwa kwao kule Namagondo, au Murutunguru, au wapi sijui kule Kisorya anatarajia maisha kuwa asali na maziwa baada ya eti kumpeleka mwana shule lakini anakuja kukatishwa tamaa mtoto ameelimika kazi hapati na hata akipata anapata kazi ya mshahara wa kijungu jiko kazi zote nzuri zinakwenda kiukoo.
Nikidhani mamake Kasri angali ameambukizwa ugonjwa na wanajamii. Hajui kwa nini mwanawe mwenye elimu na mwerevu angali maskini akilinganishwa na yule kijana mwenzake.
Nia yake kumpa elimu kijana wake ilikuwa apate kazi atajirike siku za usoni. Hii ndiyo ndoto kizazi kinachopita kimelazimishwa kuota na viongozi wa bara la Afrika. Aghalabu utawasikia wakisema...
" wapeni watoto elimu kwani mnawajengea msingi mzuri wa maisha.."
Lakini ukweli unabakia kwamba kazi zinazolingana na elimu sampuli ya kijana Kasri zinapewa wana wa walio katika uongozi.
Vile vile babake kasri hawezi kutambua sababu ya wastaafu kutollipwa marupurupu yao. Alidhani Jumuiya ya Afrika Mashariki ni mahali pema pa kufanya kazi. Lakini haiwezekani iwapo viongozi wana mtazamo tofauti na wake Kasri.