Tarehe 2/06/2006 10:19 AM, Mtoa Maoni:
Tarehe 2/06/2006 12:09 PM, Mtoa Maoni: John Mwaipopo
Nikishafanya 'kwiz' kesho nitakuwa nimekwisha kusanya ufahamu yakini kuhusu namna mlungula ulivyoshadidiwa katika awamu ya tatu ya utawala wa Bongo.
Kwa sasa ntawapa mfano mdogo tu. Kuna mwalimu mwenzangu kule TIA Mbeya (zamani DSA) ambaye hukengeusha uneni "Rushwa ni adui wa haki" na kuuita "Rushwa ni rafiki wa haki".
Hasemi tu hivihivi. Hapana. Mara zote hukazia hoja yake hii na jinsi Tanzania ilivyo kwa sasa. Huainisha upatikanaji wa huduma anuai kama vile umeme, maji, afya, polisi na kadhalika. Ukitaka kupata moja ya huduma hizo hapo kwa kufuata utaratibu husika itachukua mwaka moja ama miwili. Kama ni hospitalini si wewe ama ndugu yako atakuwa amekufa? Sasa unapotumia rushwa unapata umeme kwa siku mbili tu, maji siku hiyohiyo na kadhalika.
Hoja yangu hapa ni kuwa rushwa ama ufisadi kama inavyoitwa kule Kenya imeoteshwa mizizi hata sasa inaonekana ni sahii kushiriki na ni haramu kuwa msafi. Yoote hii kwa sababu ya kufumba macho kwetu.
Tarehe 2/07/2006 8:40 AM, Mtoa Maoni: Jeff Msangi
Tarehe 2/09/2006 1:00 AM, Mtoa Maoni: Indya Nkya
Unajua kuna matatizo mengine hayahiyaji nadharia kushughulikia. Kama alivyosema mmojawetu hapo juu kilichofanywa na serikali ya Mkapa ni kuunda taasisi kibao ambazo ziliitwa za kupambana na rushwa. Wakaandika juzuu na majuzuu kuhusu nadharia ya rushwa na namna ya kuikabili. Wakapata fedha toka kwa wafadhili. Miaka kumu ikaisha kwa kuwa na majuzuu bila upambanaji wowote wa rushwa.
Tarehe 2/09/2006 1:53 AM, Mtoa Maoni: Reggy's
Kauli ya Jenerali Ulimwengu haikumwagiwa petroli na kuporwa uraia, wala kurejeshewa kurejeshewa uraia kwa mbinde baada ya wapenda haki kulalamika.
Ni kauli yake ya muda mrefu na kwa taarifa yako, ndiyo iliyochochea apokonywe uraia wake. Ukisoma kitabu chake Rai ya Ulimwengu' kilichokusanya makala zake zote alizotoa kwenye Gazeti la Rai miaka ya nyuma, utajua kuwa kichwa chake hakipendi ufisadi.
Naamini ni kweli Serikali ya Mkapa iliendekeza Rushwa. Mkapa hakupenda kusikiliza malalamiko ya wananchi dhidi ya mteule wake yeyote. Ngoja tuone JK
Tarehe 2/09/2006 9:33 AM, Mtoa Maoni: boniphace
Tarehe 2/15/2006 7:59 AM, Mtoa Maoni: FOSEWERD Initiatives
Kasri, kuna wakati ilifika ikahojiwa kuwa PCB imekuwa ikitafuna hela bila output...labda sasa JK ataielekeza majukumu yake!
juzi wamekamata polisi nadhani tunduru kala rushwa ya 10,000 / = eti mtu kampiga mwenzie, jamaa kenda shtaki, polisi katoka kenda kuriaresti rijamaa, walipofika polisi majamaa yakakubaliana yakamalize ishu nje, polisi akayadai chau chau naona cha usumbufu wakaenda kumletea ya moto!!!! ja ja hapo mnasemaje wandughu!! na imetangazwa kweli!!!
Kuhusu swala la rushwa kumalizika nchini Bongo ndugu yangu Makene ni ndoto kwani mikono yawanaopiga kelele juu ya mapambano dhidi ya ufisadi huo imekithiri.Inasadikiwa ndiyo hao hao wanaong'ata na kupuliza.Ndiyo hao wanaopinga wala rushwa huku wakipokea na kutowa rushwa.