Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Wednesday, February 01, 2006
KAPUYA KATIKA KASHFA NZITO
GAZETI moja la Kiingereza nchini Tanzania limechapisha habari juu ya Waziri mpya wa Ulinzi Purofesa Juma Kapuya kutumia dege la jeshi katika safari zake binafsi kwenda kwao Tabora. Tukio hilo limeisababishia wizara hasara ya zaidi ya shilingi za Kitanzania milioni 10. Waweza soma habari hii zaidi hapa na kutoa maoni yako.

Kumbuka tu nchini Kenya kuna wimbi la matumizi ya fedha za serikali visivyo ambalo sasa napo limezaa kujiuzuru kwa Waziri wa fedha kama inavyofafanuliwa zaidi hapa.
 
© boniphace Tarehe 2/01/2006 12:10:00 PM | Permalink |


Comments: 1


  • Tarehe 2/02/2006 12:16 AM, Mtoa Maoni: Anonymous Anonymous

    Hahah!! Kaka Makene. Watu wanalalamika kuna njaa, mtu anakwenda na ndege kusalimia,Si bora angebeba na chakula na kudondosha kwa wenye njaa. Hivi waziri kama huyo anawaza kwamba kuna wananchi wanakufa njaa kweli!! (Binadamu wote ni sawa na Afrika ni Moja) Yeah right!!

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved