Tarehe 2/18/2006 3:42 PM, Mtoa Maoni: Jeff Msangi
Tarehe 2/18/2006 9:22 PM, Mtoa Maoni:
Tarehe 2/19/2006 1:37 PM, Mtoa Maoni: John Mwaipopo
Nikiwa naunga hoja ya kutafuta neno la kiswahili, nakupinga kuwa tumekuwa tukitumia 'blogu' kutokana na 'bogger'. Hawa blogger.com wamechukua advantage ya maana ya 'machapisho binafsi huria'. Kwa maana hii hata hao wa wordpress nao wanablogu tu (They still 'blog') Hata wa Mike Mushi nao wana-'blog'. Mfano wako wa Mobitel, Tritel, Vodacom nk hauswihi hapa. Kublog manaake kuchapisha huria mtandaoni, iwe kutumia kampuni yoyote iwayo inayotoa huduma hii. Tazama neno blog kwenye kamusi yoyote ya Kizungu uliyonayo.Kuwa na blogu yako hakuna maana yoyote ya kutumia blogger.com pekee
Tarehe 2/19/2006 1:45 PM, Mtoa Maoni:
Tarehe 2/19/2006 11:37 PM, Mtoa Maoni: mwandani
Tarehe 2/20/2006 6:05 AM, Mtoa Maoni: nyembo
Ahsante Mwandani sasa tunakoelekea ni kwenye ubishi!
Mimi sipendi hulka ya kuunga mkono hoja katika utafutaji wa jambo muhimu kama hili, bado hatujashindwa kupata maneno muafaka kwa uteuzi wa nen hilo tumiko linalotarajiwa, naomba sasa turudi katika quicktopic na kuchagua maneno muafaka na kisha kuyapigia kura bila kutumia ushabiki, kwa kuwa tukiweka ushabiki hakika tutaipoteza jamii husika itakayotumia neno hilo....naona neno muafaka kwa kulitumia ni TANDOPEPE
ALAMSIKI
Tarehe 2/20/2006 6:31 AM, Mtoa Maoni:
Kasri asante sana kwa kutukumbusha. Najua watu bado tuna nia ila tunakuwa tumetingwa na kukamatwa huku na kule.
Nitapenda kuandika usiku kirefu maoni yangu juu ya maneno ambayo yamependekezwa. Ila kwa sasa nitapenda kukubaliana na Mwaipopo kuwa neno blogu halikutokana na huduma ya jamaa wa blogger/blogspot. Huduma za blogger, wordpress, livejournal, typepad, n.k. zote ni huduma za blogu. Jamaa wa blogger waliamua kutumia neno "blog" kuweza kutangaza huduma yao lakini hili neno sio lao na wala hawakuanzisha wao. Neno hili ni ufupisho wa neno la awali ambalo ni "weblog." Kwahiyo anayetumia blogger, anayetumia wordpress, anayetumia typepad, anayetumia livejournal wote ni wanablogu kwahiyo hakutakuwa na haja ya kutafuta jina kwa kila huduma tunazotumia. Fani ina jina moja, ila huduma tunazotumia zina majina mengi.
Tarehe 2/20/2006 7:31 AM, Mtoa Maoni:
Sidhani kuwa kuna kosa kwa Mwaipopo kuendeleza mjadala. Jambo tunalozungumzia ni jipya hivyo kuna mengi ya kufunzana, kuwekana sawa ili tufikie makubaliano. Ni vyema kufikia makubaliano mapema ila hakuna sababu ya kukimbizana maana mjadala huu wa neno hautuzuii kuendelea kufaidi matunda ya teknolojia yenyewe. Tusiwe kama serikali zinavyopenda kupitisha miswada bungeni haraka haraka bila majadiliano kwa mapana na marefu. Mimi namshukuru Kasri kwa kutuamsha. Nadhani safari hii tuamue kutilia maanani. Kama nilivyoahidi hapo juu nitaandika maoni yangu juu ya maneno ambayo tumeyatoa.
Tarehe 2/22/2006 6:46 AM, Mtoa Maoni: MICHUZI BLOG
Tarehe 2/24/2006 5:37 AM, Mtoa Maoni: FOSEWERD Initiatives
kwa sababu muda mrefu umeishapita na jina mwafaka limekuwa halipatikani kwani jina blogu limekuwa linafunika jitihadi zetu. naunga mkono hoja ya Makene kuziita hizi mambo zote jina moja iwe world press (ambayo nashindwa kutoa maoni) au blogu! historia inaonyesha kuwa jina hutumika isivyo hadi ikajulikana maana halisi. nani alijua Hayati maana yake ni ALIYE HAI? nani alijua kuwa UKWASI ilikuwa inatumika ilivyo na ni kinyume na UKATA?
nikisema hivyo naomBa kutoa hoja! GAZETI TANDO ITUMIKE RASMI KUANZIA LEO NA JINA MAHUSUSI ZAIDI LITAPOTOKEA LITAJADILIWA NA KUANGALIWA KUPITISHWA!
Tarehe 3/09/2006 8:06 AM, Mtoa Maoni:
Makene nadhani jina au neno gazeti tando ndio liwe muafaka kwa hivi sasa.Naunga mkono kulipitisha na pengine kuanza kulitumia.Tusiwe kama wanasiasa,linalowezekana leo lisingoje kesho waungwana.