Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Friday, February 03, 2006
ACHANENI NA KUNYANYASA WANAWAKE

PICHA hii nadhani ingekuwa muwali sana kutumika kwa Damija maana yeye maudhui ya Gazeti Tando lake linajadili haya. Lakini hata katika KASRI suala la haki za jinsia zote hupewa kipaumbele na kuthaminiwa. Hapa hakuna unyonyaji na wala hakuna kuangalia unyanyasaji na udhalilishaji unapewa mianya katika jamii. Picha hii pia niliipata pale Carleton na niliichukua kwa hisani ya wasomaji wa Kasri la Mwanazuo.
 
© boniphace Tarehe 2/03/2006 11:37:00 AM | Permalink |


Comments: 2


  • Tarehe 2/03/2006 2:59 PM, Mtoa Maoni: Blogger Mija Shija Sayi

    Nakumbuka bwana Nyembo alishawahi kusema kwa bwana Mkwinda "mwanzo wa moto ni cheche, hivyo apokee cheche ili azibariki ziwe moto"

    Na mimi Da'Mija ninasema, Makene na wanaume wengine duniani pokeeni cheche hizo na mzibariki kuwa moto. Hao wachache wameanza na nyie wengine malizieni.

    Tupo pamoja.

     
  • Tarehe 2/03/2006 4:18 PM, Mtoa Maoni: Blogger Mija Shija Sayi

    Makene umenifanya niwafuatilie watu hawa na nikawapata hapa.
    http://www.whiteribbon.ca/about_us/

    Haya wana-Kasri pateni habari zaidi hapo juu.
    **Neno "Kasri" linapendezapendeza mdomoni kuchukua nafasi ya neno Blogu.

    Shukrani.

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved