Tarehe 1/23/2006 10:07 PM, Mtoa Maoni: nyembo
Tarehe 1/24/2006 4:13 AM, Mtoa Maoni: mloyi
majambazi motoPolisi wanajiuliza hao majambazi wamepata wapi moto huo? nao wameiga. Simama kama hutaki risasi! wengine wanasema Wao wanakamata na kuhukumu wenyewe. Fikiria ukikamatwa na kesi ya ujambazi, ambayo adhabu yake ni miaka 30 jela!, halafu polisi aliyekukamata anakupa mia tano kwa heshima anakuomba ukamnunulie sigara mtaa wa pili! utadhani ni dhali la mentali ujaribu bahati yako kukimbia huo ndio utakuwa mwisho wako huko mbele wameshajipanga na mabunduki yao , jaribu uyapechakula. Siku hizi wajanja wakipewa bahati hiyo wanakataa katakata!
Tarehe 1/24/2006 9:46 AM, Mtoa Maoni: boniphace
Tarehe 1/24/2006 4:31 PM, Mtoa Maoni: boniphace
Kaka bado akina hawa wanaojifanya kubandika makala za kuchoma katika makasri, mabaragumu, majikomboe, maharakati, manuru akilini, mamwandani nk wakijulikana tu wajiandalie makabuli maana sasa rahisi sana kuwatia mauti kwa kisingizio cha ujambazi. Tena ndugu yangu Mwaipopo usijisumbue kununua gari maana hilo ndilo litatumika kukubeba kukupeleka mazikoni. Jamani tena hakuna wa kuweza kutuhepusha na balaa hili. Sijui ngoja nifikiri upya...
Tarehe 1/25/2006 3:26 AM, Mtoa Maoni: nyembo
Tarehe 1/25/2006 6:47 AM, Mtoa Maoni: Fikrathabiti
Kikwete ameunda tume ya uchunguzi. sasa asije akala matapishi yake mwenyewe!!!Wakati akihutubia bunge aliweka wazi kua kuna ulazima wa kuzitoa taarifa za tume za uchunguzi hadharani ili waungwane waweze kujua kinagaubaga wa uzembe na uozo uliopo katika utendaji wa kazi wa vyombo vya dola.
Hii kwake ni changamoto kwahiyo tusubiri kwa mara ya kwanza kuona vigogo wakiadhibiwa kwa uzembe ulio wazi baada ya kuvumiliwa kwa mda mrefu!!
Tarehe 1/29/2006 10:52 AM, Mtoa Maoni: Ndesanjo Macha
Ujambazi, risasi, damu, vifo na mengine yanayoendana na kasi hii ya vijana wanaotaka nao kufaidi keki ya nchi ni sehemu tu ya vielelezo vya kitu Boniphace kaita, "kupanuka kwa wigo wa walio nacho na wasionacho." Sasa wawekezaji wanataka kuanza kuwekeza kwenye magereza kama ilivyo nchi mbalimbali duniani. Gereza linamilikiwa na kampuni binafsi. Hivyo ili hiyo kampuni ipate faida, inapaswa kupata wafungwa wengi. Hivyo uhalifu unakuwa ni aina ya kitega uchumi.
Mbona bado hatujaona mambo?
Hili la tume...Tanzania kwa tume naivulia kofia. Lakini matokeo ya hizi tume ni nini hasa? Tume hutufanya tuamini kuwa tatizo linashughulikiwa. Kumbuka Mkapa alivyokuja kwa mbio za tume ya rushwa...rushwa ndio ikaongezeka ikaingia hadi ikulu kwake.
Vipi umeshindwa kutafsiri Lugha hiyo ya kigeni ili isomeke katika Lugha ya kiswahili na kwa nini hukutuomba radhi wasomaji wako tuondokane na tegemeo letu kuwa tutasoma jambo kwa KISWAHILI badala yake tukakuta tutasoma Lugha hiyo ya Wakoloni?
jaribu kututhamini zaidi sisi tupendao kupitia katika blog yako haswa kwa furaha ya matumizi ya Lugha adhimu ya Kiswahili