Tunapoamua kuunda wizara sasa ya kushughulikia usalama wa Raia kwani Tanzania iko vitani sasa? Tunaogopa nini kutazama Historia na je kwani Mrema amekufa hadi tuogope kumrejeshea madaraka kama tunaona tumeshindwa kupambana na uhalifu?
Sherehe ya Boxing Day jijini Toronto iliendana na vijana wakora kurushiana risasi na kisha moja ya risasi hizo kumdhuru mpita njia aliyekuwa binti mbichi kabisa...inauma sana Michuzi! Picha hiyo inaonyesha eneo tukio hilo la kinyama lilipotokea. Nilichopendezwa nacho ni moyo wa kuthamini utu ambapo jamii nzima inajitokeza kutoa pole na kuweka mashada ya maua kwenye eneo la tukio. Nchini Tanzania ili upate heshima na huruma ya jamii ni pale unapokuwa kigogo au mtoto wa kigogo lakini jamii ya kawaida maskini wakifa hata kama ni kutokana na ujambazi husindikizwa na ndugu zao na serikali kubaki kimya.