Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Tuesday, January 10, 2006
MREMA YUKO WAPI?

Tunapoamua kuunda wizara sasa ya kushughulikia usalama wa Raia kwani Tanzania iko vitani sasa? Tunaogopa nini kutazama Historia na je kwani Mrema amekufa hadi tuogope kumrejeshea madaraka kama tunaona tumeshindwa kupambana na uhalifu?

Sherehe ya Boxing Day jijini Toronto iliendana na vijana wakora kurushiana risasi na kisha moja ya risasi hizo kumdhuru mpita njia aliyekuwa binti mbichi kabisa...inauma sana Michuzi! Picha hiyo inaonyesha eneo tukio hilo la kinyama lilipotokea. Nilichopendezwa nacho ni moyo wa kuthamini utu ambapo jamii nzima inajitokeza kutoa pole na kuweka mashada ya maua kwenye eneo la tukio. Nchini Tanzania ili upate heshima na huruma ya jamii ni pale unapokuwa kigogo au mtoto wa kigogo lakini jamii ya kawaida maskini wakifa hata kama ni kutokana na ujambazi husindikizwa na ndugu zao na serikali kubaki kimya.
 
© boniphace Tarehe 1/10/2006 01:02:00 PM | Permalink |


Comments: 0


   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved