Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Saturday, December 03, 2005
ZI WAPI HATI ZA MUUNGANO? NI MALI YA NANI? ZINAFICHWA KWA SABABU IPI?

MOJA ya matukio niliyoyapenda katika safari yangu Washington Capitol ni kukuta majengo ya kumbukumbu za ujenzi wa taifa la Marekani. Kuna piccha nimeweka kwenye albamu yangu na nyingine nitaziweka baadaye. Jingine ni hili la kukuta maandishi yajulikanayo kama Decoration of Independence. Haya yamechapishwa kabisa na kuwekwa makubwa ukutani.

Maandishi hayo yalikuwa makubaliano ya awali kabisa ya kuunda muungano wa kujenga taifa la Marekani. Tanzania na Unguja zikaungana mwaka 1964 lakini sasa tuko mahakamani kutafuta maandishi ya Muungano huo. Kweli ulifanyika Muungano unaoimbwa kumilikiwa na CCM na kama wanataka kuudumisha nini kisa cha kuficha hati ya Muungano huo.

Kuna yapi yanayofichika katika hati hiyo au Muungano huo ni geresha. Kama wazohili ni sadifu basi inawezekana Tanganyika ikawa sawa na Marekani inalazimisha kuwa na makoloni Afghanistan na Iraki. Kama ni hivyo Zanzibar inahitaji uhuru wake na hili halina siku nyingi. Uongo na usiri umegubika muungano wa mataifa haya. Tatizo hili limejenga hali ya kutokuaminiana. Tazama kufungiwa kwa Tanzania Daima kisa kuchapisha katuni yenye picha ya mfalme wa Tanzania. Haya ni mambo yanayohatarisha amani ya Tanzania. Kunyimwa haki ya kuchambuana na uhuru thabiti wa kuzungumza na kutamka yachomayo moyo.

Kuna wengi waishio katika hatihati kutokana na kusimamia haki zao na kutamka ukweli juu ya Wafalme wa Tanzania wakiongozwa na Mkapa. Kazi ipo kwako nami tunaodhani ni haki yetu kupayuka kila lifanywalo na wafalme wa Bongo. naapa siachi ng'o, bora kumaliza safari hii ya maisha mapema kuliko kudhalilisha mapenzi ya moyo wangu. Nitasema kweli daima fitina kwangu ni mwiko.

Pembeni ni mnara wa kumbukumbu wa moja wa Mababa wa taifa la Marekani na Rais wa Kwanza wa nchi hiyo George Washington. Mnara huu upo Washington D.c.
 
© boniphace Tarehe 12/03/2005 10:21:00 AM | Permalink |


Comments: 0


   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved