WANAKASRI, nikusalimu, poleni kwa kunikosa kidogo...ni suala la vimajukumu vinanitinga kwelikweli lakini nimekumbuka kupita kukusalimuni. Katika pita pita yangu nimekutana na makala hii naomba isome mwenyewe kwenye kiunganishi hiki.
Kama hizi ndizo kampeni na lugha za magazeti ya Tanzania nadhani ningeanza kufungia hili kabla sijayatazama mengine. Tazama nyingine hii na isome hadi mwisho. Oooh mbona unaniziba mdomo...samahani sisemi kama ni gazeti la serikali ya CCM. Kama haya ndiyo tunayopanda, siku si nyingi...naomba mnisamehe kutabiri huko tuendako!
Makene,
Hii ndio taswira kwenye mboni ya jicho letu la habari.Sina mengi kwa sasa,nashiriki kwenye mkutano wa Global Voices,London kupitia IRC.Ila jambo moja tu,sielewi huyu bwana Mhando anachokisema ni nini.Baadaye