SI kawaida yangu kubandika habari fupi fupi lakini imenidi kufanya hivi kwa haraka haraka. Nipo vijijini na hiki kinaitwa Newfoundland nje kidogo ya Ottawa. Hivi ni vijiji vya Ulaya si kama kwetu na hapa nipo kwenye mtandao kuandika mada hii. Phabian Mjarifu atanisamehe kwa kuchelewa kutangaza blogu hii ya kwanza kuzaliwa katika nyumba aliyozaliwa Nyerere. Amekuja nami namkaribisha sana ili aweze kutupa hizi Tafakari za maisha kutoka hapo Musoma. Nadhani nafahamu nini kilichonifanya kushindwa na kutokana na leo kufanikiwa kuwa na viungo nimeweza kuja naye harakaharaka.
Wakati Tafakari za Maisha akiingia kuna mwezetu iliyenibidi kumpiga dongo baada ya kukimbia lakini sasa karudi tazama mavituvitu yake hapa. Nakushukuru Miruko kwa kurudi maana nilikukosa sana. Usikimbie hata kama Kikwete atakupa majukumu aah mzee Malecera maana unakaa naye karibu hapo anaweza kukuchukua umuanzishie blogu lake atakaloliita uzee busara.
Wakati hayo yakiendelea, hali ya Muungano wa Tanzania inazidi kusafiri na safari ya mashua. Inaweza isifike lakini kama ukweli ni kuwa hakuna hati za Muungano nini maana ya Muungano huo. Sasa ,jadala huu kabisa bado mbichi, Ndesanjo toka likizo njoo tuanze kazi.