Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Saturday, December 24, 2005
TAFAKARI ZA MAISHA, MIRUKO NA HATI ZA MUUNGANO
SI kawaida yangu kubandika habari fupi fupi lakini imenidi kufanya hivi kwa haraka haraka. Nipo vijijini na hiki kinaitwa Newfoundland nje kidogo ya Ottawa. Hivi ni vijiji vya Ulaya si kama kwetu na hapa nipo kwenye mtandao kuandika mada hii. Phabian Mjarifu atanisamehe kwa kuchelewa kutangaza blogu hii ya kwanza kuzaliwa katika nyumba aliyozaliwa Nyerere. Amekuja nami namkaribisha sana ili aweze kutupa hizi Tafakari za maisha kutoka hapo Musoma. Nadhani nafahamu nini kilichonifanya kushindwa na kutokana na leo kufanikiwa kuwa na viungo nimeweza kuja naye harakaharaka.

Wakati Tafakari za Maisha akiingia kuna mwezetu iliyenibidi kumpiga dongo baada ya kukimbia lakini sasa karudi tazama mavituvitu yake hapa. Nakushukuru Miruko kwa kurudi maana nilikukosa sana. Usikimbie hata kama Kikwete atakupa majukumu aah mzee Malecera maana unakaa naye karibu hapo anaweza kukuchukua umuanzishie blogu lake atakaloliita uzee busara.

Wakati hayo yakiendelea, hali ya Muungano wa Tanzania inazidi kusafiri na safari ya mashua. Inaweza isifike lakini kama ukweli ni kuwa hakuna hati za Muungano nini maana ya Muungano huo. Sasa ,jadala huu kabisa bado mbichi, Ndesanjo toka likizo njoo tuanze kazi.
 
© boniphace Tarehe 12/24/2005 05:33:00 PM | Permalink |


Comments: 0


   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved