Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Sunday, December 18, 2005
NIMEFIKA CANADA
SAFARI yangu kuja Canada naweza sema imekamilika. Nimeingia Canada baada ya visa kaisi. Nilicheleshwa kufika San Antonio kutokana na askari wa Mipakani kuingia katika basi letun mara kwa mara na kutukagua. Fahamu kuwa nilitoka ukanda wa Mexico na nchi hiyo imekuwa ikiingiza wananchi lukuki Mrekani. Sababu ni kuwa Marekani inachangia umaskini wa nchi hiyo hali inayowafanya raia wake kukimbilia Marekani kila kukicha.

Nilipofika pale nikapewa ndege ya kusubiri saa kama tisa hivi. Nikapita sehemu ya kukaguliwa, yakaanza...nikawekwa pembeni kwa ukaguzi zaidi. Sijui naonekana kama gaidi lakini nilikaguliwa hadin nikachukia. Sasa kuna huyu fala anaamua kunishikashika...nikaona huu mchezo hasa baada ya kumaliza nikampa nami kauli, thanks it was such a wonderfull massage! Ananitazama kwa hasira la kufanya hana nami nachoma ndani.

Kuingia Canada kulikuwa na shida, maswali kadhaa mengi nayajibu lakini kuna binti anasema kuwa nimeonekana kujjali zaidi sheria za Marekani na kukiuka hizi za Canada. Moja sina visa, wakati nilishaambiwa kwa matembezi mafupi sihitaji visa kuingia Canada na Mexico...wengi wamesafiri hivyo lakini kwangu mimi nimekwaa kisiki. Nimekalishwa saa kama mbili huku nikikaguliwa hiki na maswali mengi. Nayajibu sasa kisiasa huku nikitangaza na nia yangu ya kuwania Ubunge mwaka 2010 kwa huyu binti ili ajue Tanzania kwangu ni nchi ila suala sasa ni mtaji wa kufikia huo Ubunge na nimeashaanza na Blogu. Haya niache hizo propaganda, usumbufu umeisha naingia nche kwenye kifusi cha barafu. Kweli Jeff alisema na nimeyaona hapa. Nafika nyumbani na mwenyeji wangu, mkarimu huyu na kisha naanza kubandika maandishi haya huku nikijiapiza kuandika waraka mwingine kuashiria utamu wa barafu hii katika shairi.
 
© boniphace Tarehe 12/18/2005 12:00:00 AM | Permalink |


Comments: 6


  • Tarehe 12/18/2005 5:04 AM, Mtoa Maoni: Anonymous Anonymous

    Haya Mzee Akida tuambie "visa kaisi" ndio nini.

     
  • Tarehe 12/18/2005 6:49 AM, Mtoa Maoni: Blogger Jeff Msangi

    Makene,
    Karibu sana Canada.Pole kwa usumbufu wa mpakani.Marekani na Canada siku hizi hazielewani vizuri tangu 9/11.Sheria za maingiliano zinazidi kuwa ngumu katika pande zote mbili,hususani kwa wasio wakazi wa kudumu katika nchi hizi.Tuwasiliane unipe programu yako.Ukiweza tafadhali tutembelee huku Toronto

     
  • Tarehe 12/18/2005 7:05 AM, Mtoa Maoni: Anonymous Anonymous

    Mambo mengine muwe mkiandikiana kwenye barua pepe.

     
  • Tarehe 12/18/2005 10:16 AM, Mtoa Maoni: Anonymous Anonymous

    Sasa waandikiane kwenye barua pepe ili wafiche uozo uliopo? Bonny hajavunja sheria yoyote na hivyo hapaswi kunyamaza pale anapoona haki yake ya msingi inapokwa. Wewe fikiria masuala ya kukaguliwa mithili ya nini sijui. Kadhalilishwa kinamna. Kama walitaka si wangesema kwa mfano anahitaji viza ya Canada. Bony hakuja Marekani kujipendekeza kama walivyo wengi ambao hawataki hata kujitambulisha kuwa wanatoka Bongo ili waendelee kubanisha Marekani kiharamu. Bony weka humuhumu kwenye blogu (neno sahihi kwa 'blog')

     
  • Tarehe 12/18/2005 11:00 AM, Mtoa Maoni: Blogger boniphace

    Tukinyamaza tutaonyesha tumeridhika na malipo ya madhila. Tukisema twaambiwa tufichiane katika barua za intanenti ili ajue Jeff tu na Mwaipopo. Kwenye Blog tunaandikia nwenzangu ambao hawayajui haya ili wajifunze na wajue kesho yakiwakuta watatue vipi. Huu ni msingi wa hulka njema za Kasri na wakazi wa Zuoni wamepata heshima nyingi kwa Qudusi kutokana na wao kupenda kuwa mawakala wa taarifa njema. Nakumbuka na kukariri tena, nitasema kweli daima fitina kwangu ni mwiko

     
  • Tarehe 12/18/2005 11:40 AM, Mtoa Maoni: Blogger Ndesanjo Macha

    Safari njema. Kama kuna theluji huko usiache kwenda kuteleza thelujini. Wewe uliwahi kuteleza kwa kisigino kwenye barabara ya udongo wakati wa masika?

    Hizo bugudha za kusachiwasachiwa na kuulizwa maswali ya ajabu ninazifahamu. Ninaelewa kabisa kilichokusukuma hata kuandika. Inaudhi sana. Wao wakija nchi zetu, visa zenyewe wanaomba na kupewa kupitia njia ya posta. Sisi kuingia nchi zao inakuwa kama kosa la jinai. Kinachoudhi kingine ni kile cha kutengwa na watu wengine uwanja wa ndege. Wengine wanaachwa wapite, wewe unaambiwa nenda pembeni. Eti wanasema tarakilishi imeonyesha kuwa unatakiwa kusachiwa kwa undani zaidi...bladifuu!

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved