Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Saturday, December 10, 2005
MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA

NIMEKUWA katika hamu ya kuona Katiba ya Tanganyika inabadilishwa. Katiba iliyopo haikidhi matakwa ya wengi. Imechoka na kubwa zaidi imejaa viraka. Mfumo wa kuunda sheria Tanzania una ukakasi. Sheria zaanzia serikalini na kisha kupelekwa bungeni kupitishwa. Hakuna kwa dhati kile kiitwacho mgawanyo wa madaraka.

Kuna haya madaraka ya Wakuu wa Mikoa na wale wa Wilaya. Vyeo hivi katika ulimwengu wa sasa havina kazi zaidi ya kuongeza mazingira ua ufalme wa watawala wa Tanzania. Kuna haja ya vyeo hivyo kutumika vingine au kuundwa kwa Bunge lenye sehemu mbili yaani lile la wawakilishi wanaotokana na majimbo yaliyopitishwa kwa uwiano wa namba ya wakazi na lile la pili litakalofanana na kuwa na wawakilishi wa aina ya wakuu wa mikoa au mithili ya maseneta ila hawa wanachaguliwa na wanannchi wa sehemu husika. Hii ni hoja ambayo amekuwa nayo mgombea wa CHADEMA, Freeman Mbowe lakini kwa muundo mwingine.

Kama kutakuwa na wawakilishi wa aina hii kunakuwa na uwezekano wa sheria mbovu zinazogandamiza haki za raia kutopitishwa. Tena ni rahisi kuwa na uwiano wa kimaendeleo badala ya sasa Mawaziri kubadilishia miradi ya maendeleo katika majimbo yao ya uchaguzi ili kujijenga kisiasa na kisha kuyadhibiti majimbo ya wapinzani kwa kuyanyima huduma za maendeleo.

Picha hiyo hapo ni Kongresi ya Marekani ambapo tulitembelea hivi karibuni. Marekani ni moja ya nchi zenye Bunge lenye sehemu mbili. Yaana sehemu ya Wawakilishi na Seneti.
 
© boniphace Tarehe 12/10/2005 10:11:00 AM | Permalink |


Comments: 2


  • Tarehe 12/12/2005 8:28 AM, Mtoa Maoni: Blogger Jeff Msangi

    Makene,
    Mfumo huu unaouzingumzia hapa ni mzuri sana ingawa lazima tuwe makini sana katika utekelezaji wake.Unajua hawa wenzetu wamedumu kwa miaka mingi sana,wana uhuru wa zaidi ya miaka mia nne sasa.Tanzania bado ni taifa changa sana ukilinganisha na Canada,Marekani au wakoloni wa dunia nzima Uingereza.Lazima tujiulize maswali kama hivi kwanini mfumo tulionao haufanyi kazi?Mfumo wetu wa kiuchumi ni ujamaa au ubepari?

     
  • Tarehe 12/12/2005 10:00 AM, Mtoa Maoni: Blogger boniphace

    Jeff nakubaliana nawe, hoja yangu inakuja kuhusiana na madaraka haya ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya. Vyeo hivi sasa vinatumika kulindana na havina kazi za msingi jambo linalotia hasara taifa. Kuna uwezekano wa kutumia vyeo hivyo na kuvipa nguvu ya kuweza kuwa na nguvu ya kutazama kila jambo linalofanywa na serikali tofauti na sasa. Nguvu za Seneti katika nchi zinazotumia Bicameral Legislatures ina umuhimu sana hasa katika mataifa yaliyoathiliwa na tabia za Kifalme Tanzania ikiwa mojawapo.

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved