Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Thursday, December 29, 2005
KARIBU BARAGUMU, BLOGU MPYA INAYOFUNGUA MWAKA
NIMEFIKA Toronto njiani nilifarijika kukaa kiti kimoja na ndugu ya jamaa huyu. Tumelonga sana nitamshtukiza na picha ili ajue raha ya blogu inavyotuunganisha. Nimefika kwa mwenyeji wangu wa awali kabla sijamtafuta mheshimiwa Waziri Mkuu si Lowasa Edward aliyechaguliwa na Kikwete kulinda urafiki wao bali huyu katika Blogu za Watanzania.

Ninapofungua barua pepe zangu nakutana na Blogu jipya kabisa la ndugu Mwaipopo. Mnamjua huyu amekuwa mchangiaji wa mada katika Blogu kwa muda mrefu. Sasa amekuja na Baragumu lake hili hapa.

Mwaipopo karibu, umekuja kipindi muwali najua hili ni blogu la kwanza kuandaliwa katika mazingira tofauti tofauti maana maandalizi yalianzia New Jersey na sasa limefunguliwa Alabama.
 
© boniphace Tarehe 12/29/2005 11:43:00 AM | Permalink |


Comments: 1


  • Tarehe 12/31/2005 2:26 AM, Mtoa Maoni: Blogger Christian Bwaya

    Ndesanjo amekuwa akisistiza sana umuhimu wa mawazo mbadala. Nafikiri ujio wa Mwaipopo utatuletea cahnagamoto zaidi katika hili.
    Makene Umechangia sana kumkaribisha bwan ahuyu katika meza hii ya duara. Kazi nzuri mzee!

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved