NIMEFIKA Toronto njiani nilifarijika kukaa kiti kimoja na ndugu ya jamaa huyu. Tumelonga sana nitamshtukiza na picha ili ajue raha ya blogu inavyotuunganisha. Nimefika kwa mwenyeji wangu wa awali kabla sijamtafuta mheshimiwa Waziri Mkuu si Lowasa Edward aliyechaguliwa na Kikwete kulinda urafiki wao bali huyu katika Blogu za Watanzania.
Ninapofungua barua pepe zangu nakutana na Blogu jipya kabisa la ndugu Mwaipopo. Mnamjua huyu amekuwa mchangiaji wa mada katika Blogu kwa muda mrefu. Sasa amekuja na Baragumu lake hili hapa.
Mwaipopo karibu, umekuja kipindi muwali najua hili ni blogu la kwanza kuandaliwa katika mazingira tofauti tofauti maana maandalizi yalianzia New Jersey na sasa limefunguliwa Alabama.
Ndesanjo amekuwa akisistiza sana umuhimu wa mawazo mbadala. Nafikiri ujio wa Mwaipopo utatuletea cahnagamoto zaidi katika hili.
Makene Umechangia sana kumkaribisha bwan ahuyu katika meza hii ya duara. Kazi nzuri mzee!