Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Thursday, December 01, 2005
HII NI ISHARA GANI
NIMEKARIRI shairi hili baada ya mwanablogu Jeff kushindwa kutimiza ahadi yake ya kutukariria shairi kila wiki. Alisema hapa, uongo sitaki tajia. Kisha sasa katokea, kizungu kufungulia. Nimekumbuka sikia, alitaka amshiwa, hivyo nami narejea kwa shairi kutungia.

SIKU ya kwanza kuanza, mwaka mpya kukamata
Macho yangu yanacheza, na tumbo kulia mbwata,
Nimeshindwa kuchomoza, mtihani kukamata
Hii ni ishara gani, kwa mwaka niloanzia?

Mwenyewe nilijapiza, mtiahani kufanyia
Wengine walishajaza, D.C nikitembea
Leo mwayo nimepaza, mlango shindwa fungua
Hii ni ishara gani, kwa mwaka niloanzia?

Nikakimbilia lulu, maktaba tafutia
Huko akaja kaburu, Blogini kunitia
Nikashindwa kumdhuru, hivyo nyumbani rudia
Hii ni ishara gani, kwa mwaka niloanzia?

Njaa ikanitafuna, shibe bora kuwazia
Nikenda viazi tafuna, utamu nikakosea
Nikakumbuka Musoma, mama akivipikia
Hii ni ishara gani, kwa mwaka niloanzia?

Jana ilikuwa jana, kila mtu kuchekea
Majini tulichuana, hakuna aloshindia
Bahari ilijazana, kama Kana tukanywea
Hii ni ishara gani, kwa mwaka niloanzia?

Salamu nikazipa, kwa wengi mpaka mamia
Simu ikawa yalia, kila dakika sawia
Blogu niposomea, salamu nikakutia
Hii ni sihara gani, kwa mwaka niloanzia?

Za intaneti barua, nyingi nimepokelea
Ndugu zangu wa Kanada, hawa napata sifia
Kila moja kakimbia, ujumbe kunandikia
Hii ni ishara gani, kwa mwaka niloanzia?

Melisa akanambia, hii ni ngao sikia
Ni moja inatokea, kwa mwaka hivyo julia
Wapaswa kuitambua, furaha yako wekea
Hii ni ishara gani, kwa mwaka niloanzia?

Najua kamba navuta, kuzimu kuelekea
Sioni mengi matata, kwani sipendi fanyia
Uchungu unonikuta, wafalme kuzidia
Hii ni ishara gani, kwa mwaka niloanzia?

Nimalize tungo tungia, nanyi mpate somea
Blogu yangu sikia, jijaze mwana tulia
Pepo yako pulizia, kila ajaye somea
Ili kesho ikifika, ashindwe kukukimbia.
 
© boniphace Tarehe 12/01/2005 06:12:00 PM | Permalink |


Comments: 0


   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved