Wednesday, December 21, 2005
ANALALAPI MIRUKO?
U wapi ndugu Miruko, zamani umepotea
Umenifanya kituko, nduguzo kuhadithia
Mbali umetupa mwiko, twakosa wa kupikia
Jamani nielezeni, Miruko amefikwani?
Mavitu nayatamani, mwezi sijayaonea
Labda ameshikwani, Keko ndani kaswekewa
Mgonjwa anawezani, mahututi kalalia
Jamani nielezeni, Miruko amefikwani?
Ya Kikwete na Nyerere, ya mwisho alitokea
Nilimtolea gere, kwa njia alopitia
Nikatamka tawire, kisa kipya pulizia
Kila nilipopitia, Miruko kanyamazia.
Nikajipa hamasiko, utulivu kachukua
Ni kosa lamba ukoko, kwa wazee najulia
Lakini kaka Miruko, Dodoma kalalia
Aha yawezekana, mwanamke kamwibia.
Nikapiga darubini, machinjioni onea
Suraye sijabaini, ni wazi amepotea
Polisi nikafikani, ripoti nikatolea
Nao wakanijibia, suraye hawajatiya!
Huu ni wito wa mwisho, bloguni andikia
Hapa sitaki michosho, mwapaswa mtafutia
Kama anaye kidosho, tujue apoishia
Siwezi kimya kalia, blogiye kusinzia.
© boniphace Tarehe 12/21/2005 09:28:00 AM
|
Permalink |
-
Asante sana. Mimi nami nimekuwa najiuliza Miruko yu wapi? Majuzi aliniambia kuwa alipotea kutokana na pilikapilika za uchaguzi. Lakini safi sana "umempiga" shairi la nguvu. Wewe mashairi haya umeyahifadhi mfukoni ambapo unayachomoa kila dakika unayotaka au? Ustaadh, Malenga wa Kilwa sijui naye yu wapi.(namzungumzia: http://mkwinda.blogspot.com
-
Mimi ni msomaji wako wa siku nyingi katika blog yako, na gazeti la Mwananchi Jumapili. Unanitia changamoto sana Bwana Makene, hebu na tufahamiane sasa, au sio bwana?
-
Miruko mirukoni, nanga aipate
bloguni haonekani,wapi nimpate
nyumbaye vumbini,wadudu wapate
dodoma ukumbini,kwake ajipate.
Naingia kwake,naye haonekani
ni nini kwake,kimyani akitani
twasubiri yake,yeye hatupani
kila sikuye,mlango hafunguwini.
Ubaya hatuna,yake maneno matamu
kuyakosa manona,yake yahamu
habari hakuna,mafunzo hatujahitimu
miruko yakuna,tupe wako ufahamu.
Rejea ukumbini,nafasi yako iwazi
tupate yako maoni,yaliyowazi
mazuri usinyimani,mabayani utuwazi
kwako mavituni,bado tunakuenzi.
Asante sana. Mimi nami nimekuwa najiuliza Miruko yu wapi? Majuzi aliniambia kuwa alipotea kutokana na pilikapilika za uchaguzi. Lakini safi sana "umempiga" shairi la nguvu. Wewe mashairi haya umeyahifadhi mfukoni ambapo unayachomoa kila dakika unayotaka au? Ustaadh, Malenga wa Kilwa sijui naye yu wapi.(namzungumzia: http://mkwinda.blogspot.com