
UNAOWATAZAMA hapa ni Watanzania wanaofundisha Kiswahili Marekani kwa mwaka 2005/06 katika mpnago unaoratibiwa na Furbright chini ya State Department. Mabalozi hawa wako katika majimbo mbalimbali hapa Marekani, kutoka kushoto ni; Clara Mtei,(Frolida), Subira kabula, (Western Virginia), Jacob Lubuva(Califonia), Boniphace Mazega Makene (Texas), John Mwaipopo (New Jersey) na January Afadhali John (Ilinois).
Kukutana kwa mabalozi hawa kulifanyika hivi karibuni huko Washington D.C. Kazi yao nasikia ni njema sana na wamekuwa wakijitahidi kupaza sauti ya bara la Afrika baada ya kugundua kuwa Tanzania hii uchi kama hakuna Afrika moja huru inayokubaliana na kuheshimiana. Nawapongeza kwa masaibu wanayokabiliana nayo huko maana inapokuja suala la wewe kuwa mweusi kwa mliowahi kufika nje ya nchi mnaweza kuwa na picha njema na mlio nyumbani mwatakiwa kuamka na kuchana na ubaguzi toka katika lugha na mwatakiwa kujenga kujali watu kwa sababu ni watu na sio rangi zao. Nadhani ujumbe huu unaweza kuwa muwali kwa Mfalme wa Jamhuri ya Tanzania ndugu Benjamin Mkapa.
Na hatuishii hapo tu. Pamoja na kujifunza yaliyo mema kutoka hapa Marekani, ambayo yapo mengi tu, na kuyaacha machafu hapa hapa, kazi nyingine ni kuwafuta ujinga hawa wamarekani kuhusu mtazamo wao kuhusu Afrika. Kwa mfano fikira ya walio wengi wao kuwa Afrika ni nchi moja na kwamba bado tunaishi vichakani, taswira wazipatazo kupitia filamu wanazopelekewa, ambazo zimesheheni uwongo na uzindiki mkuu. Kisha kuwachengua tu mimi niliwaambia namiss sana kamsosi ka panya (chamaki nchanga wa kule Ntwara, ingawaje sijawahi kuonja licha ya kutamani kufanya hivyo). Halafu nimewaambia kuwa kasehemu ka ziada waliyo nayo wasisahau,wakipenda, kukainvest kwenye elimu barani Afrika badala ya kupoteza kwenye miradi hasi mingi waliyonayo.