Kasri, jumba la weledi waweza keti hapa na kupata ukitakacho. Chakula cha wakazi wa Kasri ni fikra na chakula hiki kimewapa thawabu wananchi wa nchi hii hali inayowafanya kutoziba midomo yao kila waonapo damu ya wanaonyanyaswa ikidondoka katika bahari ya dhiki, maangamizi na unyonyaji. Waweza nawe keti hapa na kula fikra hizi.
Wednesday, November 30, 2005
LEO NI SIKU YA KUZALIWA MWALIMU BONIPHACE MAZEGA MAKENE
LEO nakumbuka siku yangu ya kuzaliwa. Hili ni tukio ambalo katika mila za Kiafrika halikuwa na nafasi sana. Mara ya kwanza kwangu kufanya sherehe hii ilikuwa kidato cha sita pale Mkwawa. Mara nyingi sherehe hunikuta shuleni mbali na familia ya kwetu.

Leo hii pia imenikuta hapa Amerika na vijana wamechachamaa sana kuwa lazima kuwepo na hafla. Inaonekana itakuwa hafla kubwa tu kwani rafiki zangu walikuwa wamesafiri kila mtu kivyake kwa ajili ya sherehe za Thanksgiving. Mimi nami nilikuwa Washington D.C na kisha Houston Texas. Nilirudi hapa siku mbili zilizopita. Kazi ni nyingi lakini kwa kuwa rafiki wanahitaji kunywa Juisi ya Maembe pamoja nami nimeona siwezi kuwakatalia.

Lakini nakumbuka jambo moja ninapokuwa nakata mbuga ya siku za uhai wangu hapa duniani. Nashukuru kuwa Mwaka huu umeonesha dira halisi ya mimi kuwa kiumbe wa dunia hii. Ni jana tu nilipoanza majukumu ya kudurusu Utamaduni na Kiswahili kwa wanafunzi wangu wapendwa, wote mabinti wapatao watano hivi. Walifurahi sana jana na leo ninaadhimisha kuanza mwaka mpya.

Naanza mwaka mpya huku Tanzania wiki ijayo ikifanya uchaguzi. Najua kuwa Kikwete atashinda lakini swali langu lipo katika Baraza lake la Mawaziri. Sidhani kama atafuata urafiki kugawa madaraka. Kama akifuata hivyo basi huyu jamaa tajiri mkubwa aitwaye Lowassa anayemfuatia Sumaye atakabidhiwa kiti hicho. Lakini nimekumbuka kuna mchezo humo ndani. Yawezekana nafasi hii kama uadilifu utafuatwa akapewa Mongella. Huyu mama anafaa na \ni wazi huu ni wakati wake kuhema na kucheka katika Tanzania baada ya kutamba sana katika duru za kimataifa.

Mwaka huu murua sana maana kichwa changu kimepanuka sana katika masuala ya kisiasa. Mifumo ya mataifa haya makubwa nimejitahidi kuyasoma na kuyazingatia. KADRI SIKU ZIENDAVYO NDIVYO NINAVYOZIDI KUIVA. Siku mbili zilizopita kulikuwa na mafafali ya kuhitimu shahada ya kwanza pale Mlimani ambapo mimi nilipewa yangu. Haikuwa kama ya Mrema yangu nimeisotea kwa miaka minne na hiki ndicho kisa cha mimi kuanza jina langu na kuitwa Mwalimu Makene.

Kuanza fani ya ualimu moja kwa moja na shahada ya Chuo Kikuu ni nadra sana katika Tanzania. Wachache hao ni mimi pia. Ni wazi kazi hii nitaifanyia kazi baadaye. Nitarudi kuongeza habari hii baadaye.
 
© boniphace Tarehe 11/30/2005 06:12:00 PM | Permalink |


Comments: 5


  • Tarehe 12/01/2005 2:51 AM, Mtoa Maoni: Blogger mloyi

    Mwalimu Makene.. Nimekuwa na mawazo ya kutembelea blogu yako kwa juma zima ila nilikuwa mvivu kutafuta anuani yako,Ila leo nimefanya hivyo.
    Mwaka mpya umeanza kwako, Hongera kwa kumaliza uliopita, na umalize salama miaka ijayo..
    Natarajia utatumia mwaka huu kutupasha habari motomoto zaidi kwenye hiki kibaraza chako.

     
  • Tarehe 12/01/2005 6:13 AM, Mtoa Maoni: Blogger Ndesanjo Macha

    Hongera sana Makene kwa siku hii. Pia kwa picha ulizotupatia za walimu wa kiingereza na pia kwa Safari ya Mashua.

     
  • Tarehe 12/01/2005 8:58 AM, Mtoa Maoni: Blogger boniphace

    Nakushukuruni Ndugu zangu. Maana kila kukicha naongeza ndugu na hizi Blogu zinazidi kuwaongezeni kuwa ndugu zangu wa dhati. Nakupongezeni kwa kunipa faraja kusoma fikra zenu. Endeleeni ndugu zangu na karibuni hapa Kasirini maana nyie Wanazuo kwelikweli

     
  • Tarehe 12/21/2005 11:16 PM, Mtoa Maoni: Blogger FOSEWERD Initiatives

    Bwana makene!

    unajua saa nyingi wazungu wanatuchanganya! ni kweli viongozi wanawake ni wazuri lakini labda isipite uwezoo wa mtu kufanya kazi bila kuangalia makunyanzi! unajua katika mawaziri ambao hutenda kiushujaa tanzania lowasa ameongoza? unajua ametumia muda mwingi mbugani kuliko ofisini? si umeona alivyoshughulikia sakata la DAWASA na kuwatimua city water? si umeona jinsi alivyopambana na wamisri katika mzozo wa maji na kuwapa maji washinyanga? kuna mtu mmoja aliwahi kufanya naye kazi anadai lowasa ni wa mwisho kulala na wa kwanda kuamka! - hatakama, kama ni mwanamke si mwampe mdogodogo kama mama nagu? huyu mongela aliyefanya kazi na nyerere wa nini tena?

     
  • Tarehe 11/24/2016 11:00 PM, Mtoa Maoni: Blogger Unknown

    I 'm so glad you could come across this site ,
    and we hope to establish good relations with you.
    greetings from me ( OBAT KUAT )


    obat pembesar penis

    jual vimax

    obat kuat viagra

    jual kondom

     
   
 
Copyright 2006 © BONIPHACE MAKENE. All Rights Reserved