NIMEFIKA hapa leo na kukutana na ndugu zangu kutoka TANZANIA. Safari ya kuja huku ina lengo la kujadili masuala ya kisiasa na namna ya kujipanga kusaidia umma wa watanzania. Mazungumzo haya ya leo yanaongozwa na mtaalamu wa Udaktari anayesomea masuala hayo hapa Marekani, Mwandishi na mwongoza Picha za video na Televisheni anayechukua shahada hiyo hapa Marekani, mtaalamu wa masuala ya Kisiasa anayesoma na kufundisha hapa Marekani, na mtaalamu mwingine wa masuala ya Upasuaji naye hapa Marekani.
Mazungumzo haya yatawafurahisha sana hawa: Baraka Mraha, Selestine Kakele, Nehemia Mandia, Gasper Materu na wengine siwataji kwa sababu muhimu. Fuatilia makala zangu katika Mwananchi kupata visa hivi na wale mnaonipata hapa subirini wiki kesho maelezo zaidi.
Boniphace,
Karibu mwana kwetu. Nimo ndani ya Kasri lako dakika hii. Hongera kwa kuingia kwenye ulimwengu wa blogu.